Saturday, April 20, 2013

WATU MILIONI 14 WANUFAIKA NA HUDUMA YA MATIBABU YA MABUSHA NA MATENDE TANZANA: DK. MWELE


Dk. Mwele Malekela ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa NIMR akifungua Mjadala juu ya Utafiti wa udhibiti wa ugonjwa wa mabusha na matende kwa nchi za Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika.
Baadhi ya washiriki ambao ni watafiti wakifuatilia mada za mjadala huo.
Dk. Upendo Mwingira akitoa mada yake juu ya matumaini ya kutokomeza Ugonjwa wa Matende na Mabusha hasa kufuatia utafiti wake Wilayani Tandahimba.
Mmoja wa watafiti
Sehemu ya washiriki wakifuatilia majidiliano hayo juu ya ugonjwa wa matende na Mabusha.
Watoa mada mbali mbali kutoka nchi za Afrika wakitoa mada zao juu ya Tathmini ya ugonjwa wa Mabusha na Matende katika nchi zao.

Na Mroki Mroki wa Father Kidevu Blog, Arusha

Wilaya 94 zimefikiwa katika zoezi la unyweshaji dawa za Matende na Mabusha  na utoaji elimu linaloendeshwa chini ya Mpango wa Taifa wa Kudhibiti magonjwa yasiyopea kipaumbele (NTD) unaoratibiwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.

Mkurugenzi Mkuu wa NIMR Dakta Mwelecele Malecela ameyasema hayo mjini Arusha wakati akizungumza na waandishi wa Habari katika Kongamano la 27 la taasisi hiyo la  Sayansi la Kongamano la Pili la Afya Moja Afrika  linaloendelea mjini humo.

Dk. Malecela amesema watu milioni 14 wamenufaika na huduma ya matibabu ya mabusha na matende  katika wilaya hizo 94 ambazo zimefikiwa katika zoezi la ugawaji dawa na tiba.

Aidha alieleza kuwa katika wilaya ya pangani jumla ya watu mia mbili waliokuwa wanasumbuliwa na mabusha wamepatiwa tiba kwa njia ya upasuaji na tayari wamerejea katika hali ya kawaida na kuweza kuendelea na shughuli za maendeleo ya jamii yao.

No comments:

Post a Comment