Saturday, January 19, 2013

KAMPUNI YA GREEN WASTE PRO LTD YAZINDUA KAMPENI YA USAFI CITY CENTER JIJINI DAR ES SALAAM


Meneja Mkuu wa Kampuni ya Green Waste Pro, Elizabeth Scheepers (wa tatu kushoto), akiwa na  viongozi wengine wa kampuni hiyo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya usafi City Center maeneo ya ufukwe wa Bahari ya Hindi Barabara ya Ocean Dar es Salaam leo asubuhi. Kutoka kulia ni Msimamizi wa Kampuni hiyo Said Mazingira, Ofisa Uhusiano, Vidah Fammie, Oparesheni Meneja Abdallah Ally, Mkusanyaji wa kumbukumbu, Cindy Joyce na Joshua Palfreman ambaye alijitolea kufanya usafi katika uzinduzi wa  kampeni hiyo.
Meneja Mkuu wa Kampuni ya Green Waste Pro, Elizabeth Scheepers akishiriki kufanya usafi
Usafi ukiendelea kufanyika katika eneo hilo
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilaala Jerry Silaa (kulia), alikuwa ni miongoni mwa viongozi waliojitokeza kufanya usafi baada ya kuzinduliwa kwa kampeni hiyo.
Lundo la vifuu vya madafu vikiwa kando ya ufukwe wa Bahari ya Hindi katika eneo hilo na kuharibu kabisa mandhari ya ufukwe huo, vifuu hivyo viliondolewa katika kampeni hiyo.
Joshua Palfreman ambaye alijitolea kufanya usafi katika uzinduzi wa  kampeni hiyo akiokota takataka katika uzinduzi wa kampeni hiyo.


Na Dotto Mwaibale

MEYA wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa leo amezindua kampeni ya usafi katika jiji la Dar es Salaam hasa maeneo ya Kati kati ya jiji.

Kampeni hizo zimefunguliwa na Meya huyo na kuhudhuriwa na wadau wengine mbalimbali kutoka sekta binafsi, wananchi na viongozi wa kampuni ya Green Waste pro.

Silaa alitoa mwito kwa wakazi wa Manispaa ya Ilala kujenga  tabia ya kushiriki katika usafi wa jiji kuanzia kwenye kata na kuwa uzinduzi wa leo umehusisha Kata tatu ambazo ni Kata ya Kivukoni, Mchafukoge pamoja na Kata ya Kisutu.

"Kwa kuanzia tumeanza na kata hizi katika Manispaa ya Ilala lakini baadae zitahusishwa na  Manispaa nyingine ili kuliweka jiji katika hali ya usafi.

Uzinduzi wa kampeni hiyo ulienda sambamba na utoaji wa elimu ambayo itafanyika katika mashule mbalimbali na Taasisi nyingine ikiwa na lengo la kuhamasisha wananchi kuwa na tabia ya kujali elimu ya mazingira na maeneo yanayo wahusu.

No comments:

Post a Comment